Miamba ya kandanda nchini
HISPANIA, FC BARCELONA na SEVILLA inakabiliana usiku huu katika fainali
ya UEFA SUPER CUP inayopigwa BORIS PAICHADZE DINAMO ARENA, MJINI
TBILISI, GEORGIA
Mchezo huu unaowakutanisha
Mabingwa wa UEFA CHAMPIONZ LIGI na waliobeba UEFA EUROPA LIGI, ndio
unaoashiria kuanza rasmi kwa Msimu mpya wa Soka Barani Ulaya.
Mechi hii ya kusisimua inaanza kupigwa kuanzia Saa 3 Dakika 45 Usiku huu kwa saa za Afrika mashariki.
FC Barcelona wanatinga Uwanjani
bila ya nyota wake wa Brazil Neymar, huku wakisaka kuifikia rekodi ya
AC Milan ya kutwaa mara tano UEFA Super Cup.
Mbali ya kumkosa Neymar, ambaye
nafasi yake inachukuliwa na Pedro anayedaiwa kuhamia Manchester United
baada ya Mechi hii, Barca, chini ya Kocha Luis Enrique, pia inawakosa
majeruhi Jordi Alba na Douglas.
Wachezaji wapya, Arda Turan na
Aleix Vidal hawaruhusiwi kucheza hadi Januari kwa vile hivi sasa Barca
ipo kwenye Kifungo cha FIFA cha kutosajili.
Hii ni mara ya pili mfululizo kwa
Sevilla kugombea UEFA Super Cup baada ya kutetea vyema Taji lao la
EUROPA LIGI lakini Mwaka Jana kwenye Fainali hii walichapwa magoli
mawili kwa bila dhidi ya Real Madrid.
No comments:
Post a Comment