22 July, 2015

VIDEO ikimuonesha Straika wa Napoli, Gonzalo Higuain akizinguana na watu mjini Ibiza, Hispania.

CKg5tv8UkAAGVs6Kuna video moja imeonekana leo ikimuonesha Straika wa Napoli, Gonzalo Higuain akizinguana na watu mjini Ibiza, Hispania.
Kwa mujibu wa ripoti, video hiyo ilirekodiwa alfajiri ya leo wakati nyota huyo mwenye miaka 27 akiondoka katika klabu moja ya usiku inayojulikana kwa jina la Pacha iliyopo kisiwani humo.
Higuain alikuwa anakula bata na mshambuliaji wa PSG, Ezequiel Lavezzi katika klabu hiyo, wanaripoti El Mundo.
Baada ya mshambuliaji huyo kuamua kurudi nyumbani, alizingirwa na mashabiki ambao walitaka asaini autograph, lakini Higuain alikataa na kuanza kuzinguana nao mpaka kufikia hatua ya kutaka kupigana.
Higuain alishikwa na mlinzi wake, na alipogundua tuko lile limerikodiwa alifoka kwa sauti:
“Futa video vinginevyo nitakupasua kichwa”.
Hata hivyo tukio hilo halikuendelea….Tazama video hapa chini:

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...