18 July, 2015

Manchester United wanajiandaa kumuachia David De Gea kama mchezaji huru msimu ujao kuliko kumuuza kwasasa kwenda Real Madrid.

david-de-gea-training-in-seattleMan United wameweka masharti kwamba De Gea atauzwa Real Madrid majira haya ya kiangazi endapo miamba hiyo ya Bernabeu itakubali kuwauzia mlinzi wa kati, Sergio Ramos.
Kumbuka De Gea na Ramos wote wapo katika timu zao kujiandaa na msimu mpya.
Kocha mpya wa Real Madrid, Rafa Benitez amesema hataki tu Ramos abakie Bernabeu bali anataka kumpa kitambaa cha unahodha kufuatia Iker Casillas kuondoka.
Kwa mujibu wa The Guardian, inasemekana dili la Ramos kutua Old Trafford linaweza kukamilika kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili la Majira ya kiangazi.
United hawana presha ya kuuza wachezaji kwenda klabu kama Real Madrid kwasababu wana mkwanja wa kutosha kuweza kuwazuia wanasoka wake.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...