25 July, 2015

MAKALA: HIFADHI ZA WANYAMA TULIZO NAZO NI UZURI TOSHA WA TANZANIA

serengeti-park
             Na Francis Mawere.
Ni matumaini yangu yakwamba uu mzima na nipende kukupatia pole kwa mihangaiko ya hapa na pale. 
 Leo ningependa kidogo kuongelea juu ya HIFADHI ZA WANYAMA TULIZO NAZO HAPA KWETU. 
  Ni kweli kabisa TANZANIA ni nchi iliyo barikiwa kuwa na vivutio vingi vya utalii vikiwepo vileee vya hifadhi za wanyama. pata kuvijua hii leo.
   
 Hifadhi ya Serengeti
 Hifadhi ya Serengeti ni eneo kubwa la mbuga na misitu katika Tanzania ya kaskazini hasa katika mikoa ya Mara na Arusha ikipakana na nchi ya Kenya.
Eneo lake ni 14,763 km² na kijiografia inaendelea ndani ya Kenya inapoitwa Hifadhi ya Masai Mara.
Kuna idadi kubwa ya wanyamapori. Serengeti pamoja na Masai Mara inajulikana hasa kwa uhamisho wa kila mwaka wa zaidi ya milioni moja ya nyumbu wanaovuka mto Mara. Kuna pia aina nyingi nyingine za wanyama, kati yao "watano wakubwa" wanaovuta watalii hasa yaani tembo, simba, chui, fisi, kifaru na nyati.
Eneo la hifadhi ya Ngorongoro liliwahi kuwa sehemu ya Serengeti hadi kutengwa kama hifadhi ya pekee. Bonde la Olduvai ambako mabaki ya zamadamu yalipatikana liko ndani ya Serengeti.
Mazingira ya Serengeti ni kanda ya kijiografia katika kaskazini-magharibi mwa Tanzania na inaenea kusini-magharibi mwa Kenya kati ya latitude 1 na 3 Kusini na longitude 34 na 36 Mashariki. Inaenea kiwango cha mraba kilometa 30,000 2.
Serengeti ina gura/uhamiaji ya wanyama kwenye ardhi kubwa na ndefu zaidi duniani,[1] ambao hua ni tukio wa nusu mwaka . Uhamiaji huo ni moja ya maajabu kumi ya asili ya ulimwengu ya kusafiri.
Kanda hii ina hifadhi za taifa na hifadhi mchezo kadhaa. Jina Serengeti limechukuliwa kutoka lugha ya Kimasai hasa, "Serengit" kumaanisha "Kiwara kisichoisha". 
Inakadiriwa mamalia 70 kubwa na baadhi ya spishi 500 avifauna (yaani ndege) hupatikana huko. Tofauti hii ya juu upande wa spishi ni shughuli makazi mbalimbali kuanzia misitu ya riverine, mabwawa, kopjes mbuga na misitu. Nyumbu bluu, swara, punda milia na nyati ni baadhi ya mamalia kubwa ambao kwa kawaida hupatikana katika kanda hii.
Karibu Oktoba, karibu wanyama wanaokula majani (si nyama) milioni 2 husafiri kutoka milima ya kaskazini kuelekea nyanda za kusini na kuvuka mto wa Mara katika harakati za mvua. Katika mwezi Aprili, wao hurejea kaskazini kwa kupitia magharibi, na kwa mara nyingine tena kuvuka Mto wa Mara. Jambo hili la mara kwa mara huitwa kwa Kiingereza "Circular migration" yaani uhamiaji mviringo. Nyumbu zaidi ya 250,000 pekee watakufa safarini kutoka Tanzania kwenda katika mbuga ya wanyama ya Masai Mara huko Kenya pande za juu, ambayo ni jumla ya maili 500. Kifo mara nyingi unasababishwa na maudhi au uchovu. Uhamiaji huu umeonyeshwa katika filamu na programu nyingi za televisheni kote duniani.

 Historia ya Hifadhi ya Serengeti
 Sehemu kubwa wa Serengeti hapo awali ilijulikana kama Maasailand kwa wageni.
Wamasai walijulikana kama shujaa wakali, na waliishi pamoja na wanyamapori huku wakila mifugo yao pekee.
Nguvu zao na sifa zilisababisha wasafiri kutoka Ulaya kutotumia wanyama na rasilimali ya nchi yao vibaya.
Janga la "rinderpest" na ukame wakati wa 1890 ulisababisha kupungua kwa idadi ya Wamasai na wanyama. Uwindaji haramu wa wanyamapori na ukosefu wa moto, ambayo yalikuwa matokeo ya shughuli za binadamu, yaliweka hatua ya maendeleo ya misitu na vichaka kwa miaka 30-50 ijayo.
Uongezekaji wa chafuo sasa ulisababisha kutokuwa kwa makazi ya binadamu katika eneo hili.
Moto, tembo, na nyumbu walikuwa na ushawishi mkubwa katika kuamua sasa muundo wa Serengeti.
Mnamo miaka ya 1960, idadi ya binadamu ilivyoongezeka, moto, aidha kuwashwa kwa makusudi na Wamaasai ili kuongeza eneo ya malisho ya mifugo, au kwa ajali, ulisababisha kuchomeka kwa miche mipya ya miti.
Mvua nzito ilichangia ukuaji wa majani, ambao ulikuwa kama mafuta kwa moto wakati wa misimu mikavu ifuatayo. Miti mizee ya Acacia, ambayo huishi tu miaka 60-70, ilianza kufa. Awali tembo, ambao hula miti michanga na mizee, walilaumiwa kwa kumaliza misitu. Lakini majaribio yalionyesha kulikuwa na sababu nyingine muhimu zaidi. Wakati huo huo, idadi ya tembo ilipunguzwa kutoka 2,460 mwaka 1970 hadi 467 katika mwaka 1986 kutokana na uwindaji haramu.
Mnamo miaka ya 1970 idadi ya nyumbu na nyati wa Afrika ilikuwa imeongezeka, na walikuwa wakipunguza idadi ya majani kwa kasi, na kusababisha upungufu wa mafuta ya kusambazaa moto. kupunguka kwa ukali wa moto umesababisha Acacia kuwa imara tena.

Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro
Mlima Kilimanjaro Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro ni maarufu duniani kutokana na mandhari nzuri ya Mlima Kilimanjaro ambao ni mlima mrefu kuliko yote Afrika na inapatikana katika nchi ya Tanzania. Hifadhi hii ina ukubwa wa kilometa za mraba 755 na iko umbali wa kilometa 45 kutoka Moshi mjini. Kilele cha Kibo chenye urefu wa mita 5895 (futi 19340) ndio kivutio kikubwa kwa wageni kutoka ndani na nje ya nchi kutokana na kufunikwa na theluji.
Mlima huu ni moja kati ya milima ambayo kilele chake hufikiwa kwa urahisi na hivyo kuwa kivutio kikubwa kwa wapanda milima kutoka kila pande za dunia.
  • Safari ya kupanda mlima huu humpitisha mpandaji katika kanda za hali ya hewa tofauti kuanzia ile ya nchi za tropiti hadi arktiki.
Zaidi ya watalii 20,000 hupanda mlima huu kila mwaka wakiwemo wageni kutoka nje ya nchi na Watanzania. Mpandaji wa mlima huu huhitaji angalau siku tano, siku tatu kupanda na siku mbili kuteremka.
Kuna njia sita ya kupanda mlima Kilimanjaro hadi kileleni.
  • Njia iliyo rahisi na maarufu zaidi ni ile ya kuanzia lango la Marangu, ambako ndiyo makao makuu ya hifadhi.
Wanyama kadhaa hupatikana katika msitu unaozunguka Mlima Kilimanjaro wakiwemo mbega, nyani, nyati, chui, tembo, swala na ndege.

Hifadhi ya Mikumi
Mikumi ni moja ya hifadhi mashuhuri na kubwa nchini Tanzania. Eneo kuu na muhimukatika hifadhi hii ni uwanda wa mafuriko pamoja na safu za milima ambazo zinapatikanandani ya hifadhi hii. Mbuga za wazi ndizo zinazoshamiri katika uwanda wa mafuriko na kuishia katika misitu ya miombo inayofunika mabonde yaliyo chini ya hifadhi.
Twiga ndani ya Hifadhi ya Mikumi
Hifadhi hii ina ukubwa wa kilometa 3230 na ipo umbali wa kilometa 283 magharibi mwa Dar ea Salaam. Aidha hifadhi hii iko kaskazini ya mbuga ya Selouse na iko njiani unapoelekea katika hifadhi ya Udzungwa, Selouse na Ruaha kwa barabara kutoka Dar ea Salaam na Inapatikana katika Mkoa wa Morogoro.
-Ndani ya hifadhi ya Mikumi kuna simba ambao huwa wanaonekana wakiwa katika himaya yao na mara nyingine wakiwa juu ya matawi ya miti ili kukwepa majimaji wakati mvua zinapototesha ardhi ambayo ina udongo wa mfinyanzi.
-Wanyama wengine wengi hukimbilia katika eneo la miombo nyakati za mvua ambako unaweza kuwaona katika safu za milima. Hapo makundi makubwa ya nyati katika ukanda wa miombo wanaweza kuonekana.
-Kwa upande wa ndege, wakati wa mvua huongezeka na kufikia zaidi ya aina 300. Hii ni kutokana na ukweli kwamba, nyakati hizi kunakuwepo na makundi ya ndege wahamiaji kutoka nchi za Ulaya na Asia ambayo, huungana na makundi ya ndege wakazikama vili chole.
-Makundi makubwa ya viboko, pundamilia na nyumbu huonekana katika eneo hili.

  Ni matumaini yangu umeweza kufahamu Mbuga zetu maarufu zinazoipa Nchi yetu Uzuri unao washusha UDENDA na kumeaza MATE wazungu. Nipende kukushkuru ww uliechukua muda wako wa thamani kuipitia MAKALA hii.
    
OMBI LANGU KWAKO 
Tuipende Nchi yetu, na mali zake zote kwani ni nchi pekee inayofaa.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...