14 July, 2015

Lil Wayne karushiwa chupa na Birdman night club akashtukia.. tukio lilirekodiwa kwenye hii video.

lil wayneKwa muda mrefu sasa hivi kumekuwepo na beef kati ya rapper Lil Wayne na Birdman wa Cash money na hii ni baada ya Wayne kujitoa Cash Money kwa kutoridhishwa na ishu kadhaa ikiwemo kutosikilizwa anachotaka hasa kwenye ishu ya album yake kucheleweshwa kutoka.
lil wayne 2
Picha za tukio lenyewe, Lil Wayne akishangaa kurushiwa chupa alafu kwenye hii ya kulia ndio birdman anaonekana na timu yake.
Baada ya kujitoa Cash Money, Wayne ameendelea na show zake kama kawaida ambapo weekend iliyopita alikuwepo Miami Marekani kwenye club moja ya usiku ambapo kumbe na ‘mbaya wake’ Birdman nae alikuwepo tena akimtazama Lil Wayne kwa chini wakati akiperform.
Inadaiwa Birdman alirusha kwa Lil Wayne chupa ya kinywaji alichokua anakunywa na kusababisha show kusimama kwa sekunde chache huku watu wakijiuliza chupa imetoka wapi lakini badae ndio ikaja kujulikana kwamba Birdman ndio aliirusha.
Hivi vipisi vya video vinaonyesha hiyo moment kwenye hili tukio.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...