03 June, 2015

Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF leo limezindua jezi mpya za timu za Taifa,

MALIZI3
Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF leo limezindua jezi mpya za timu za Taifa, zitakazokuwa zikitumika na timu za Taifa katika michuano mbali mbali itakayokua inazikabili.Uzinduzi huo wa jezi mpya uliofanyika katika ukumbi wa Kilimanjaro jengo la Golden Jubilee uliambatana na uziduzi wa tovuti mpya ya
shirikisho, uliongozwa na mgeni rasmi Mh. Said Mtanda, mbunge wa jimbo la Mchinga na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya jamii. Katika uzinduzi huo, kulizunduliwa jezi aina tatu, ambazo ni jezi za ugenini, jezi za nyumbani na jezi zitakazokuwa zikitumika kwa ajili ya mazoezi.
Ifuatayo ni hotuba ya Rais wa TFF , Jamal Malinzi aliyoisoma wakati wa uzinduzi wa jezi mpya za timu za Taifa, uzinduzi wa tovuti mpya ya TFF na kutunuku vyeti kwa viongozi mbalimbali, makocha, wachezaji na wadhamini.
Mh Said Mtanda Mbunge wa Jimbo la Mchinga na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii
Mzee Said el Maamry Mwenyekiti Msataafu wa FAT
Ndugu Leodeger Tenga Mjumbe wa Kamati ya utendaji ya CAF na Rais mstaafu wa TFF
Ndugu wageni waalikwa
Ndugu waandishi wa habari
Mabibi na mabwana
Salam aleikum.
Nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutufikisha hapa leo na kwa mafanikio mbali mbali ambayo tumekuwa tukiyapata.Ninakushukuru sana ndugu mgeni rasmi kwa kuacha shughuli zako kuja kujiunga nasi asubuhi hii katika shughuli hii.
Ndugu mgeni rasmi,tarehe 08 oktoba 1964 Tanzania ilipata uanachama rasmi wa shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA. TFF tuliona jambo zito kama hili hatuwezi kuliacha lipite hivi hivi.Hivyo mwaka jana tuliamua kuenzi  maadhimisho ya miaka 50 ya kujiunga na FIFA kwa kufanya mambo mambo matatu makubwa.
La kwanza ni kutoa vyeti maalum kwa watu binafsi na taasisi mbali mbali kwa kutambua mchango wao uliotukuka katika kuendeleza mpira wa miguu Tanzania.
Leo hii ndugu mgeni rasmi tutakuomba ukabidhi vyeti hivi kwa wawakilishi wa makundi kadhaa kwa niaba ya wenzao.Makundi haya ni pamoja na viongozi wa kitaifa wastaafu,mawaziri wa michezo wastaafu,viongozi waliopita wa TFF?
FAT,wakurugenzi wa idara ya michezo,wenyeviti na makatibu wa baraza la michezo la taifa,Timuya Taifa iliyocheza fainali za Afrika mwaka 1980,waamuzi,makocha,wachezaji wa timu ya Taifa na watangazaji mahiri wa michezo.Jumla tumetunuku vyeti 194.
Kiuhalisia idadi hii ni ndogo sana ukilinganisha na wingi na uzito wa michango ya wadau mbali mbali wa mpira katika miaka 50 iliyopita.
Tunaomba Watanzania wenzetu watuelewe katika hili kuwa hawa tutakaowatunuku vyeti hivi ni wawakalilisha wa wadau wote wa mpira Tanzania.
Ninaomba tusimame kwa muda mfupi tuwaombe ewadau wenzetu na viongozi wa mpira wa miguu ambao wako katika orodha hii na wametangulia mbele ya haki.
Ndugu mgeni rasmi katika kuenzi miaka 50 ya Tanzania kujiunga na FIFA leo hii pia tutatoa mchango wa fedha kwa makundi yenye mahitaji katika jamii.
Pesa hizi zinatokana na makusanyo mbali mbali ikiwemo makusanyo ya mechi ya ngao ya hisani ifanyikayo kila mwaka. Makundi haya ni pamoja na walemavu wa viuongo,walemavu wa ngozi na wasioona.
Kitendo hii ni moja ya juhudi za TFF kurudisha katika jamii kile tunachokusanya. Kila kundi litapewa shilingi milioni tano na tunaendelea kupokea maombi toka makundi mbali ya kijamii na tukiyapitisha tutaendelea kugawa fedha hizi.
Jambo la tatu tutakalolifanya leo litakuwa ni kuzindua rasmi tovuti mpya ya TFF (www.tff.or.tz). Tumeamua kufanya jamabo hili katika kuenzi miaka hamsini ya kujiunga na FIFA ili kutoa msisitizo kuwa sasa TFF na sisi tunajiunga Na kuendeleza mpira kisasa kulingana na teknolojia iliyopo.
Kupitia tovuti hii wadau wa mpira watapata fursa ya kuhabarishwana kuelimishwa nkuhusu masuala mbali mbali yahusuyo mpira wa miguu.
Tovuti hii itakuwa pia na sehemu ya kumbu kumbu (archive) zihusuzo historia ya mpira wa miguu na matukio mbali mbali katika historia ya mpira wetu.
Tunaomba wadau wenye kumbu kumbu mbali za mpira kama picha,takwimu,vipande vya magazeti ya zamani na kadhalika mtuletee ili viingizwe katika tovuti yetu.
Tunaamini tovuti hii itakuwa ndio chanzo kikuu cha taarifa na rekodi mbali mbali za sasa na za zamani  zihusuzo mpira wa miguu.
Ndugu mgeni rasmi shughuli ya leo tutaihitimisha kwa kuzindua jezi mpya ya timu ya Taifa. Jezi hizi zitakuwa ni mbili moja ya ugenini na nyingine ya nyumbani.Tunawapongeza watanzania wote walioshiriki katika kubuni jezi na mwisho tuliunganisha ubunifu tofauti na kupata jezi itakayozinduliwa leo.
Ubunifu huu tayari umetafutiwa hati miliki Brela hivyo TFF tutalinda hakii hii kwa kuwakamata na kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria wale wote watakaodiriki kuchapisha na kuuza kwa magendo jezi hizi.Utaratibu unafanyika kumpata msambaji mmoja halali atakayesambaza jezi hizi nchini kwa ajili ya wapenzi wa mpira wa miguu.Ukinunua jezi hii utakuwa umechangia maendeleo ya mpira wa miguu.
TFF inawashukuru na kuwapongeza sana Tanzania Breweries ltd ambao ndio wazalishaji wa bia ya Kilimanjaro Lager kwa sapoti wanayoitia kwa timu ya Taifa na kutuwezesha kubuni na kuzalisha jezi hizi.Tunawashukuru sana.
Ndugu mgeni rasmi ninaomba nimalizie kwa kuzungumzia kwa kifupi program yetu ya mpira wa vijana.kwa kutambua umuhimu wa kuendeleza soka la vijana TFF tumejipanga vilivyo kwa mpambano wa hatua za awali za kucheza fainali za vijana za Afrika umri chini ya miaka 17 mwaka 2017.
Mechi za ufaulu zitafanyika kati kati ya mwaka 2016.TFF tayari tumeunda kikosi cha awali cha vijana chini ya umri wa miaka 15 kujiandaa na michuano hii.Kikosi hiki kimetokana na michuano ya copa coca cola ya mwaka jana.
Tunapenda tuchukue fursa hii kumshukuru Rais Dr Jakaya Mrisho Kikwete kwa kufanikisha nchi yetu ya Tanzania,kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi hii,kupata uenyeji wa fainali za Afrika. Shirikisho la mpira wa miguu Afrika CAF limeipatia Tanzania uenyeji wa fainali za Afrika za vijana umri chini ya miaka 17 mwaka 2019.
Tunaomba Serikali itushike mkono katika hili ili tuweze kuandaa mashindano mazuri.Lakini haitakuwa vyema Tanzania kuandaa mashindano mazuri lakini tukatolewa hatua ya makundi.Siku ya jumapili tarehe 07/juni TFF tutazindua mashindano ya taifa ya vijana umri chini ya miaka 13 mjini mwanza.
Wachezaji bora wa mashindano haya ndio wataunda kikosi cha awali cha Taifa kwa ajili ya kushiriki fainali za Afrika watoto umri chini ya miaka 17 mwaka 2109.
Tunaomba Serikali pamoja na wadau wote tushirikiane katika kukilea kikosi hiki ili mwaka 2019 tuwe na timu nzuri.
Tunamshukuru Mh Dr Fennela Mukangara na wizara nzima ya habari vijana utamaduni na michezo kwa ushirikiano wanaotupatia katika hatua hizi na katika shughuli nyingine za kuendeleza mchezo wa mpira wa miguu.
Ndugu mgeni rasmi ninaomba sasa nikukaribishe uhutubie hafla  hii na pia utuongoze katika shughuli zitakazofuata.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...