Mwigizaji wa siku nyingi na nyota wa filamu zilizopendwa na wengi Sir Christopher Lee amefariki akiwa na umri wa miaka 93.

Msanii huyo ambaye ni mzaliwa wa Uingereza aliyejenga jina lake kwa
kuigiza katika filamu ya Dracula na Frankenstein katika filamu ya
kutisha aligiza katika zaidi ya filamu 250.Alijulikana sana kwa kuigiza kama Scaramanga katika filamu ya James Bond
na Evil Wizard Suriman katika filamu ya
Lord of the Rings.
Msanii huyo pia ameigiza katika filamu za The Wicker Man na Stars wars.
Inaripotiwa kuwa mwigizaji huyo alifariki siku ya jumapili katika
hospitali ya Chelsea Westminster mjini London baada ya kulazwa na
ugonjwa wa tatizo la mapafu na moyo.
No comments:
Post a Comment