08 June, 2015

Mabingwa wapya wa Ulaya klabu ya FC Barcelona inajiandaa kumtangaza kiungo Aleix Vidal

Aleix-Vidal-Sevilla1
Mabingwa wapya wa Ulaya klabu ya FC Barcelona inajiandaa kumtangaza kiungo wa pembeni wa FC Sevilla, Aleix Vidal kama ingizo jipya katika klabu hiyo baada ya kukamilisha usajili wake siku ya jumamaosi.

Licha ya kuwa katika kifungo cha kutosajili mpaka mwaka 2016, mabingwa hao wa Hispania na Ulaya wamekuwa katika harakati za kunasa saini kadha wakadha kwa ajili ya kuboresha kikosi chao ingawa watatakiwa kusubiri hadi Januari 2016 ili kuanza kuwatumia wachezaji hao.
Aleix Vidal amesaini mkataba wa miaka 5 na Barcelona siku ya Jumamosi baada ya klabu hizo mbili kukubaliana juu ya ada ya uhamisho inayotajwa kufikia pauni milioni 10.
Winga huyo anayeweza kucheza pia nafasi ya mlinzi wa pembeni, anatarajiwa kuwa nyongeza na mbadala sahihi wa beki wa Kibrazil Dani Alves ambaye licha ya juhudi za raisi wa klabu hiyo Josep Maria Bartomeu kumbakisha Camp Nou, anaonekana kuikaribia milango ya Old Trafford na kufata nyayo za Victor Valdes aliyejiunga na mashetani wekundu hao msimu uliomalizika.
Mhispania huyo aliyesajiliwa na Sevilla msimu uliopita akitokea Almeria alikocheza michezo 120 na kufanikiwa kupachika wavuni mabao 17, ameichezea Sevilla michezo 31 msimu huu na kufumania nyavu mara 4 huku akitengeneza mabao 11 na kuisaidia vilivyo Sevilla katika mafanikio yake ya kombe la Europa msimu huu.
Sasa Vidal atatambulishwa rasmi siku ya jumatatu kwenye mkutano maalumu na waandishi wa habari kama mchezaji halali wa wafalme hao wa bara la Ulaya baada ya kufaulu vipimo vya afya.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...