12 May, 2015

TIMU TATU ZINAZO WINDA SAINI YA MTOTO WA PODOSKI MWENYE UMRI WA MIAKA 7.

3,w=993,c=0.bild
LUKAS Podolski, mshindi wa kombe la dunia akiwa na timu ya taifa ya Ujerumani mwaka jana nchini Brazil ambaye kwasasa yupo kwa mkopo Inter Milan kutokea Arsenal amehojiwa kuhusu mtoto wake na kufichua kuwa anazivutia klabu nyingi.
Mtoto huyo mwenye miaka 7 anayeitwa Louis Podolski, kwasasa yupo katika kituo cha watoto cha Bambini cha Inter na Podolski ametangaza kuwa klabu tatu za Ujerumani zinajaribu kuiwinda saini ya mtoto wake ili ajiunge na timu zao za vijana.
Timu hizo ni Cologne, Bayer Leverkusen na Borussia Mönchengladbach.
Podolski amesema: “Mtoto wangu sasa ana miaka 6 kuelekea saba, anaichezea Bambini (Inter). Tayari ameshanasa kwenye rada. Sasa Cologne, Leverkusen na Gladbach wanahitaji kumsajili. Katika umri huu, inashangaza!”
Podolski alijiunga kwa mkopo na Inter katika dirisha dogo la usajili mwezi januari mwaka 2014 na anatarajia kurejea Arsena mwishoni mwa msimu huu.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...