12 May, 2015

Muingereza Stewart John Hall Arejea tena AZAM FC

Stewart-John-Hall
Taarifa kutoka  chanzo cha kuaminika ndani ya klabu ya Azam fc zinaeleza kuwa kocha wa zamani wa klabu hiyo, Muingereza Stewart John Hall anarejea tena kuwa kocha mkuu.
Hall aliyeiacha Azam fc baada ya kumalizika kwa mzunguko wa kwanza wa ligi kuu msimu wa 2013/2014 anarejea kuchukua mikoba ya aliyekuwa kocha mkuu, Joseph Marius Omog.
Omog alifukuzwa kazi mwezi februari mwaka huu baada ya Azam kutolewa ligi ya mabingwa Afrika  na El Merreick kwa ushindi wa jumla wa magoli 3-2 na nafasi yake ikachukuliwa kwa muda na aliyekuwa kocha msaidizi, George ‘Best’ Nsimbe.
Kwasasa Nsimbe ndiye kocha mkuu wa muda na msaidizi wake ni Dennis Kitambi, hivyo kurejea kwa Hall kuna maanisha kocha mmoja anaweza kuwa msaidizi wake.
Nsimbe ameshindwa kutetea ubingwa aliochukua Omog msimu uliopita.

Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO, SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>Zawadi_mawere. SuScribe Youtube>>>MAWERE TV.

 

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...