29 May, 2015

SEPP BLATTER KASHINDA TENA AWAMU YA PILI

BLA
SEPP BLATTER ameshinda kwa mara ya tano kiti cha Urais wa Shirikisho la soka duniani FIFA baada ya kupata kura 133 dhidi ya 73 za mpinzani wake Prince Ali bin Al-Hussein katika raundi ya kwanza ya uchaguzi mkuu uliomalizika usiku huu mjini Zurich, Uswizi.
Blatter mwenye miaka 79 alipata ushindi katika raundi ya kwanza  na kabla ya kwenda raundi ya pili, Prince Ali alijitoa.
Baada ya kushindwa  katika uchaguzi huo, Prince Ali amesema: “Nashukuru nyote. Imekuwa safari ndefu na ya kushangaza. Asanteni kwa wote mliopnipigia kura”
Changamoto aliyonayo Blatter ni kukabiliana na Skendo ya rushwa ya dola milioni 100 inayowakabili maafisa sita wa ngazi ya juu wa FIFA.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...