16 May, 2015

MFAHAMU KOCHA ATAKAE ICHUKUA NAFASI GORAN PALE SIMBA

455624-9bf08b2b290f79e5baa009dba4ee85d9 (1)
GORAN Kopunovic bado anaihangaisha Simba kuhusu kusaini mkataba mpya na aliahidi kutoa jibu jana ijumaa, lakini bado amekuwa mgumu kuweka wazi kama amekubali au la! kuendelea na kibarua chake Msimbazi.

Sababu inayofanya Simba washindwane na Kopunovic mpaka  sasa ni Mserbia kutaka mshahara mkubwa wa dola za Kimarekani elfu tisa (9,000) sawa na shiloingi milioni 18 za Kitanzania.
Pia anataka dau la kusaini la dola za kimarekani elfu hamsini (50,000) sawa na shilingi million 100 za Kitanzania.
Siku za karibuni, mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe alikaririwa na vyombo vya habari akisema wanasubiri maamuzi ya Kopunovic ambaye kwasasa yuko likizo Hungary na kama atakataa kukubali ofa yao basi watatafuta kocha mwingine kurithi mikoba yake.
Hans Poppe na viongozi wenzake kwa siku nzima ya jana walikuwa wanasubiri jibu la Kopunovic, lakini mpaka usiku hakukuwa na taarifa yoyote kutoka kwa kocha huyo mwenye mbwembwe nyingi anapoiongoza timu yake.
Hata hivyo taarifa mpya iliyotolewa na Bin Zubeiry asubuhi ya leo inasema kocha Mbelgiji, Piet de Mol atatua Dar es Salaam Mei 21, mwaka huu kwa ajili ya mazungumzo ya kuifundisha Simba SC, lakini kutua kwa kocha huyo kutategemea na msimamo wa mwisho wa Simba SC juu ya Goran.
 Kwa mujibu wa mtandao wa Wikipedia, De Mol mwenye umri wa miaka 60 ana uzoefu mkubwa wa kufundisha soka Afrika, Asia na Ulaya na alikuwa nchini Ghana akifanya kazi ya Mkurugenzi wa Ufundi wa akademi mjini Kumasi. Pia  alifanya kazi na Asante Kotoko. Pia alifundisha timu ya kwao Ubelgiji, Dubai, Qatar na China. Alikuwa kocha Msaidizi wa AA Gent kuanzia mwaka 1997 hadi 2001.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...