01 May, 2015

Louis van Gaal anaamini msimu ujao Man United itachuana na Chelsea kuwania ubingwa

28349BB700000578-3064249-image-m-45_1430487750925
Louis van Gaal anaamini msimu ujao Man United itachuana na Chelsea kuwania ubingwa 
Louis van Gaal anaamini msimu ujao Manchester United itapambana vikali na mabingwa watarajiwa wa ligi kuu England, Chelsea katika mbio za ubingwa baada ya kukamalisha maandalizi yake ya kabla ya msimu (pre-season) yatayofanyika katika ziara ya Marekani.
 Van Gaal alikosoa ziara ya Marekani ambayo  tayari ilikuwa imepangwa kabla ya kuanza kazi yake majira ya kiangazi mwaka jana  na kwa  muda usiozidi wiki mbili aliiongoza klabu kwenda Los Angeles, Washington DC, Detroit, na Miami.
Ingawa United walishinda mechi zote za maandalizi ya msimu, Mholanzi huyo alilaumu ratiba mbaya na waliporudi England Agosti 28 kuanza ligi kuu walivuna pointi 13 tu katika mechi 10 za kwanza.Premier League giants United will face Club America, San Jose Earthquakes, Barcelona and PSGMiamba ya ligi kuu England itacheza na Club America, San Jose Earthquakes, Barcelona na PSG katika maandalizi ya kabla ya msimu

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...