20 May, 2015

HATIMAE KOCHA WA SIMBA AMEKUBALI KUPUNGUZA DAU LAKE NAKUSALIA MSIMBAZI.

GORAN-1-0
TAARIFA mpya leo zinasema kocha mkuu wa Simba aliyemaliza mkataba wake, Mserbia Goran Kopunovic amekubali kurejea Dar es salaam kuendelea na kazi ya kuwanoa vijana wa Msimbazi wenye uchu wa mafanikio kuelekea msimu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara.
Tayari Simba kupitia kwa mwenyekiti wa kamati ya usajili, Zacharia Hans Poppe walithibitisha kuachana na Kopunovic kwasababu ya kutaka dau kubwa la usajili na mashahara mrefu, hivyo kuanza harakati za kusaka kocha mpya.
Kopunovic alitakiwa kutoa jibu kufikia Ijumaa ya wiki iliyopita kama atasaini mkataba mpya au la!, lakini alishindwa kufanya hivyo.
Kopunovic alitaka dola za Kimarekani 50,000 (sawa na Sh. Milioni 100) kama dau la kusaini Mkataba na mshahara wa dola 8,000 (Sh. Milioni 16) kwa mwezi, kiasi ambacho Simba walisema hawawezi kulipa.
Sasa Mserbia huyo amekubali kushuka  dau na atarejea nchini kuanzia juma lijalo kusaini Mkataba mpya na mara moja kuanza maandalizi ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame.
Yuke kocha Mbelgiji Piet de Mol aliyeripotiwa kuja kesho kuwania nafasi ya Kopunovic, atakuja kama kawaida, lakini kutafuta kazi klabu nyingine.

Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO, SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>mawere_mtoka_mbali,SuScribe Youtube>>>MAWERE TV

 

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...