06 May, 2015

Barcelona kuifunga Beyern leo?


MTIFUANO wa Ligi ya Mabingwa Ulaya unaendelea kuwa mtamu baina ya  miamba ya soka barani humo Barcelona na Bayern München kushuka dimbani Camp Nou kwa ajili ya kutafuta tiketi ya kutinga fainali ya michuano hiyo.
Wakati hayo yakijiri vitabu vya kumbukumbu za kihistoria vya Shirikisho la Soka la Ulaya (UEFA) vinaonyesha Hispania imeendeleza rekodi yake ya kuwa na timu katika nusu fainali kwa misimu 16 ukianza msimu wa 1992/93.
Hispania imeshikilia rekodi hiyo ikikosa timu misimu 6 tu katika misimu 22  huku wawakilishi 26 kati ya 88 waliotinga hatua hiyo wametoka nchini humo.
England imeshika nafasi ya pili kwa kuwa na wawakilishi 20 kati ya 88 sawa na asilimia 22.7 ikilinganishwa na 29.5 ya Hispania.
Msimu huu ni wa tisa kwa nchi ya England kukosa timu kwenye hatua ya nusu fainali.
Italia na Ujerumani (timu 14), Ufaransa (timu 6), Uholanzi (4), Ureno (2), Ugiriki na Ukraine (1).
Uimara
Gerrard Pique amekaririwa akisema hajawahi kuona safu ya ushambuliaji kama MSN–Messi, Suarez na Neymar tangu aanze kuitumikia Barcelona.
Bayern chini ya kocha aliyeifanikisha Barcelona Pep Guardiola inatarajiwa kumiliki  mpira zaidi lakini uimara wa Bavarians upo zaidi ya hapo kwani wanaweza kucheza zaidi ya mifumo iliyonayo Barcelona.
Uwepo Roberto Lewandowski katika ushambuliaji ni faraja kubwa akiungwa mkono na Thomas Müller, Mario Gotze Frank Ribery na Jerome Boateng utaisumbua sana ngome ya Blaugrana.
Udhaifu
Barcelona ina uwezo wa kushika mchezo kama timu huku ikikosa uwezo wa mmoja mmoja (man-for-man) ambao Bayern wanao hivyo kama wote watataka kukaa na mpira basi uwezo wa Barca kusimama kwa mchezaji mmoja moja hautakuwepo.
Kwa upande wao Bayern watamkosa Arjen Roben ambaye ni majeruhi huku kukiwa na hatihati ya kumkosa Frank Ribery.
Tukirejea katika mechi mbili za Bayern katika Bundesliga iliruhusu mashambulizi ya ghafla kutoka kwa Wolfsburg na Möenchengladbach kama wasiporekebisha itawagharimu.
Rekodi ya Barcelona katika nusu fainali imepoteza mara 8 na kushinda mara 6 huku Bayern ikishinda mara 10 na kupoteza mara 6.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...