11 April, 2015

Mourinho:Kinyang'anyiro cha EPL kiko wazi

Kocha wa Chelsea Jose Mourinho
Mkufunzi wa kilabu ya Chelsea Jose Mourinho amesema kuwa kinyang'anyiro cha kuwania ubingwa wa ligi ya EPL bado kiko wazi licha ya timu yake kuwa mbele na pointi saba mbali na mechi moja ambayo haijacheza.
Mourinho anaamini kuwa timu yoyote ambayo iko nyuma na pointi saba ama nane bado ipo katika kinyang'anyiro na kwamba hashangazwi na kushuka kwa Manchester City katika kupigania taji hilo.
Chelsea itamenyana na QPR ugenini jumapili katika debi ya Magharibi mwa London.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...