11 April, 2015

BBC>>>>Kiongozi wa Muslim Brotherhood kunyongwa


Mahakama moja nchini Misri imethibitisha hukumu ya kifo ya kiongozi wa kundi la Muslim Brotherhood Mohammed Badie na watu wengine 13 kwa kupanga mashambulizi dhidi ya serikali.
Pia mahakama hiyo imemfunga maisha raia mmoja mwenye uraia wa Marekani na Misri na watu wengine 36.
Badie alipewa hukumu hiyo mnamo mwezi Machi na pia anakabiliwa na mashtaka mengine.
Hatahivyo anaweza kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo.
Mamia ya watu wamehukumiwa kifo katika msako dhidi ya wanachama wa kundi hilo kufuatia kuondolewa kwa rais Mohammed Morsi mwaka 2013.
Hatahivyo ,kufikia sasa ni mtu mmoja pekee aliyenyongwa.
Uamuzi huo wa mahakama ulitangazwa moja kwa moja na runinga za taifa hilo.
Hukumu hizo ni za mwisho katika kesi ambayo viongozi wa kundi la Muslim Brotherhood walishtakiwa kwa kuwachochea wanachama wa kundi hilo kuanzisha ghasia dhidi ya serikali kufuatia maandamano ya mwaka 2013.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...