04 April, 2015

Moroco yashinda kesi CAS.


Morocco fans_getty

KIONGOZI wa juu wa Shirikisho la soka nchini Morocco, Nour Eldin Boushehati ameweka wazi kuwa taifa lake liko tayari kuwa mwenyeji wa fainali za mataifa ya Africa, Afcon 2017.
Mahakama ya juu ya rufani ya FIFA ya masuala ya mpira (CAS)  alhamisi ya wiki hii iliitangaza Morocco kuwa huru kutoka katika kifungo cha CAF na kusema wanaweza kushiriki fainali za Afcon 2017 na 2019.
Boushehati sasa anajiamni kuwa wako tayari kuhodhi michuano hiyo kwa miaka miwili mfululizo.
“Tuko yatari kuwa wenyeji wa michuano ijayo ya Afcon  kama serikali itatupa ruksa, tuko tayari, tunaisikiliza serikali. Wakituruhusu tutakuwa tayari kuwa wenyeji,” Amesema Boushehati.
Morocco walitakiwa kuwa wenyeji wa fainali za Afcon mwaka huu 2015 lakini walichomoa dakika za mwisho wakihofia mlipuko wa ugonjwa wa Ebola.
Guinea ya Ikweta ilikubali kuwa mwenyeji wa fainali hizo muda mfupi baada ya kuombwa na CAF.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...