14 April, 2015

Flaviana Matata kaibuka tena kwenye MAGAZINE ya Kimataifa, kingine kuhusu yeye ni hiki..

Flavi
Mwanamitindo wa TZ ambaye yuko kwenye HEADLINES za Kimataifa.. Nimekutana na kitu kinachohusu yeye mtandaoni, nikaona kwa sababu ni mtu wetu basi niisogeze hii ili watu wake pia waone.
Kaingia kwenye HEADLINES za Magazine kubwa duniani, BLACK ENTERPRISE ambao wamefanya nae exclusive interview, mengi kayasema hapa
mengine hata sikuwahi kuyajua kutoka kwake.. kumbe ishu ya kuingia kushiriki Miss Universe hata hakuwa na idea ya kitu anachokifanya, aliingia kwa kujifurahisha tu !!
Kingine alichokiongea ni ishu ya Flaviana Matata Foundation, taasisi ambayo aliianzisha kwa ajili ya kusaidia wasichana yatima kwenye masuala mbalimbali ikiwemo mahitaji muhimu ya Shule.FlavianaNiliwahi kumuona marehemu mama yangu akisaidia watoto wengine kuwapeleka shule.. Nilikuwa mdogo sana lakini alikuwa akituambia na ndugu zangu umuhimu wa kusaidia watu ambao wanahitaji msaada.. Nilianzisha FMF kwa ajili ya moyo wa kujitolea..“– Flaviana Matata.
Jitihada nnazozifanya kusaidia wasichana kupata elimu itakuwa ni kitu ambacho kila mtu anaweza kukipongeza..“– Flaviana Matata.
Safari ya staa wetu wa mitindo inaendelea yani, kwenye exclusive hiyo amesema moja ya changamoto iliyopo TZ ni watu wachache kutoa support kwenye misaada anayotooa kwa kuwa ni wachache ambao wanajua maana ya kujitolea kwa jamii.
Tumeona zaidi ya mara mbili staa huyu anatoa misaada mashuleni, anahitaji support yako pia mtu wa nguvu ili kuifanikisha, unaweza kumfollow kwenye Twitter na Facebook @FlavianaMatata, Instagram unaweza kumcheki kwa kubonyeza hapa pia @


Mawerenewz.blogpot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO,SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA
Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Francis mawere the jr, Instagram>>>Zawadi_mawere. AKSANTE.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...