12 April, 2015

Dawa za kulevya:Nelly mashakani


Mshindi wa tuzo ya Grammy mwanamuziki Cornell Haynes ama kwa jina maarufu Nelly amekamatwa na shtaka la mihadarati baada ya polisi kusimamisha basi alilokuwa akisafiria mjini Tennessee nchini Marekani.
Alikamatwa kwa kuwa basi hilo halikuwa na vibandiko halali kabla ya kuchunguzwa kutokana na harufu ya bangi iliokuwa ikinuka.

Idara ya usalama na usalama wa nyumbani baadaye ilisema kuwa Nelly alipelekwa hadi Jela ya kaunti ya Putnam baada ya basi hilo kusimamishwa.
Msanii huyo wa muziki wa kufokafoka alishtakiwa na makosa ya kumiliki bangi kabla ya kuachiliwa kwa dhamana .
Mtu mwengine ambaye pia alikuwa akiabiri basi hilo alikamatwa na kushtakiwa ,mamlaka imesema.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...