04 April, 2015

Arsenal yaichapa Liverpool

arsenal  11
 Ligi kuu ya Uingereza jioni ya leo imeendelea katika viwanja tofauti nchini humo huku Arsenal ‘The Gunners’ wakiwafumua Liverpool kwa jumla ya mabao 4-1 na kufanya ndoto wa Majogoo hao wa jiji la Landon kuzidi kupoteza matumaini ya kushiriki klabu bingwa Ulaya mwakani.
Arsenal ndio walianza kupata bao kupitia kwa Hector Bellerin kunako dakika ya 37 kabla ya Ozil kucheka na nyavu dakika ya 40 baada ya kuachia shuti kali lililotokana na adhabu ndogo kufatia mchezaji wa Aresenal kufanyiwa madhambi.
Dakika ya 45 Sanchez  aliiandikia The Gunners bao la tatu kabla ya Olivier Giroud  kufunga kabisa idadi ya mabao katika uwanja wa Emirates kwa kuandika bao la 4, Bao pekee la Liverpool limefungwa na Jordan Henderson kwa mkwaju wa penati.
Katika mchezo huo Mchezaji wa Arsenal ambao walikuwa wanatumia mfumo wa (4-2-3-1) na Timu ya Taifa ya Ujerumani, Mesut Ozil, alifanikiwa kuibuka 

arsenal 666Man of the Match.Kocha wa Arsenal Mfaransa Arsene Wenger aliwatumia Ospina, Bellerin, Mertesacker, Koscielny, Monreal, Coquelin, Cazorla,  Ramsey, Sanchez, Ozil, Giroud. huku wengine wakianza benchi kama, Gibbs, Macey, Rosicky, Walcott, Welbeck, Gabriel, na Flamini.
Kikosi cha Liverpool kikiwa chini ya Brendan Rodgers ambacho kilitumia mfumo wa 3-4-2-1 kilikuwa ni Mignolet, Can 5, Toure, Sakho,  Henderson, Allen, Lucas, Moreno, Markovic, Coutinho, Sterling huku Sturridge, Borini, Brannagan, Johnson, Jones, Lovren, Manquillo wakianzia benchi.
Kuatia matokeo hayo sasa Aresenal inakuwa imeishusha Manchestar City katika nafasi ya pili ikiwa na alama 63 mele kwa pointi 2 huku wakiendelea kusoma namba za Chelsea wanaoongoza kwa alama 67.arsenal 33

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...