03 May, 2016

Huyu ndiye Gerald Levert

Nafahamu fika vijana wengi wanaotamba huku mitandaoni ni wale waliozaliwa miaka ya 90 nakuendelea, na naku-hakikishia ni Asilimia chache sana ya vijana walio katika kundi hili wano mfahamu huyu jamaa aliye julikana kwa jina la Gerald Levert ila kama wewe ni wale walio zaliwa miaka ya 80 basi haswaaa utakua na mimi sanjari.( ha ha haaa natania tuu bhana) but any way Jokes aside now tuje kwenye Mada yetu ya leo.

Linapo tajwa jina la wimbo Cassanova ama Baby Hold On to Me, basi hutoacha kumskia Gerald Levert hapo kati amakundi zima la O’Jays. Huyu jamaa alizaliwa mnamo July 13, 1966 huko Canton katika jimbo la Ohio nchini Marakani.Alikua ni mwana muziki na muigizaji. Na ali-zaliwa katika familia ya muziki ambapo mdogo wake Sean Levert ndie aliye husika katika kuundwa kwa kundi Lililo julikana kwa jina la LeVert.
Akiwa High school mnamo mika ya 1984, ndipo alipa amua kujiingiza moja kwa moja kwenye mziki ambapo aliungana na Mdogo wake Sean Levert akiwa na rafiki yake Marc Gordon na kuunda kundi la muziki walilolipatia jina la R&B trio LeVer.
Kundi hilo lilifanikiwa kuingia  studio nakurekodi album saba ambazo me mimi naziita "five scoring gold/platinum success" na Album hizo ni kama vile “I Get Hot” (1985), “Bloodline” (1986), “The Big Throwdown” (1987), “Just Coolin” (1988), “Rope A Dope Style” (1990), “For Real Tho” (1993) “The Whole Scenario (1997) pamoja na ngoma kali kama vile  “(Pop, Pop, Pop, Pop) Goes My Mind”, “Casanova”, “My Forever Love”, “Just Coolin” (featuring Heavy D), “Baby I’m Ready” and “ABC-123″ In 1991 the Group hit again with “Livin For The City”

Mnao mwaka 1991 Gerald aliondoka katika kundi hilo na kuamua kufanya kazi zake akiwa kama  solo artist na alifanikiwa kutengeneza album ambayo ilichukua namba moja katika chart za Bilbord album hiyo ilijulikana kwa jina la Private Line, na mwaka ulio fuatia aliachilia hit nyingine alomshirikisha baba yake na wimbo huo ulijulikana kwa jina la 'Baby Hold On to Me'. Gerald aliendelea kutoa album nyingi mpaka alipo fikia miaka ya 1990s na mwanzoni mwa miaka ya  2000s ambapo alipata collabo ya wimbo kama vile “Thinkin’ About It ulio achililiwa 1998 Funny”, “Mr. Too Damn Good to You”, “U Got That Love”, and a remake of R. Kelly’s 
“ I Believe I Can Fly”,

Gerald aliandika, kuproduce na kufanya kazi na wasanii kama vile Barry White, Stephanie Mills, Anita Baker, Eugene Wilde, Teddy Pendergrass, James Ingram, Freddie Jackson, Chuckii Booker, The Winans, Troop and The O’Jays. Na aliwahi kuonekana katika movies kama vile “Just Don’t Do It” pamoja na ile ya Always and Forever” zote hizo zilikua chini ya mkali Jamie Foxx.

Mnamo November 10, 2006, Gerald alikutwa akiwa amekufa kitandani mwake ambapoa aliyegundua kifo chake alikua ni binamu yake ambaye alikwenda kumuamsha. Kwa mara ya kwanza ili riptiwa kuwa kilicho muua nguli huyo ni matatizo ya moyo(heart attack) lakini taarifa kamili ya kifo chake ilitoka mwaka 2007 mwezi February ikieleza kua Gerald Aliji-overdoze na madawa. Na mwishoni ikafahamika kuwa ni sumu ya dawa hizo ili zidi kwenye damu. Alifariki na maika 40 tuu na aliacha mke na watoto watatu.

Aliacha albu yake ilokwenda kwa jina la “In My Songs” ikiwa bado jikoni iliyo achiliwa mwaka 2007 chini ya familia yake. Pamoja na Manaement iliyo kuwa ikimsimamia.

                 Tizama moja ya kazi zake huyu jamaaakiwa na kundi la LSG.


Kwa kifupi hiyo ni historia ya nguli huyo wa muziki aliye wahi kuishi ila teyari keshatangulia mbele za haki ambako mimi na wewe tutakwenda siku moja (R.I.P).

Unaweza kujipatia makala hii na makala zetu moja kwa moja kwenye simu yako kila ifikapo week-end Bure kabisa. Unacho takiwa kukifanya ni kujaza Fomu unayo iona hapo chini...

PITIA NA HIZI:-

>> Oliver Mtukudzi picha Halisi ya Muziki wa Kiafrica.
>> unalifahamu-kundi-la-ub40? 
>> Wafahamu madancer Albir Rojas na Sara Lopez wakali wa 'Kizomba dance'



Jiunge na watu 3000 walio chagua MTOKAMBALI ili kupata Makala zinazo chapishwa Hapa hapa MTOKAMBALI na kuja kwako moja kwa moja kupitia Emai yako kila week-End BURE!!

* indicates required

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...