18 October, 2016

Liverpool 0-0 Manchester United

Mchezo wa kusisimua wa ligi kuu ya soka England umemalizika kwa suluhu ya bila kufungana.

Katika mchezo huo kipindi cha kwanza timu zote zilishambuliana kwa zamu huku kipindi cha pili Liverpool ikishambulia zaidi lango la United.
Kocha wa Liverpool Jurgen Klopp amesema kuwa hakukasirika lakini pia hakufurahishwa na kiwango cha uchezaji wa timu yake. 

Klopp pia ameisifu safu ya ulinzi ya Man U na kusema ilikuwa vigumu kushinda kutokana na ulinzi ulivyokuwa imara.
Kwa upande wake meneja wa Man U Jose Mourinho amesema licha ya kutopata matokeo aliyoyataka lakini ameridhishwa na matokeo hayo.
Amesema si matokeo mabaya kwani waliweza kumzuia hasimu wao wa jadi kuondoka na alama tatu nyumbani kwake.

Katika mchezo huo Ander Herrera aliibuka kuwa mchezaji bora huku akiwa mchezaji aliyegusa mpira mara nyingi kuliko mchezaji yoyote , aligusa mpira mara tisini

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...