17 March, 2016

Serikali ya Zimbabwe yapinga marufuku ya WhatsApp

Serikali ya Zimbabwe imekataa pendekezo la kampuni za simu kupiga marufuku huduma ya Over The Top{OTT} kama vile WhatsApp na Skype ,waziri mmoja amenukuliwa katika gazeti la Herald akisema.
Kampuni hizo zilitoa ombi la huduma ya OTT zisimamiwe akihoji kwamba zinawazuia kupata faida.
''Tulisema kwamba sisi kama taifa endelevu ambalo linakuza teknolojia tunapuuza wazo hili la kuzipiga marufuku teknolojia hizi ,waziri wa habari na teknolojia Supa Mandiwanzira alisema.
Wabunge nchini Afrika Kusini pia wamekuwa wakilijadili ombi hilo la makampuni ya simu kusimamia huduma hizo za OTT ambazo zinaonekana kuwa rahisi kwa matumizi

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...