20 March, 2016

Mfahamu Msanii Eddy Kenzo

12592457_563038880520506_7295650620544001446_n
Edrisah Musuuza kwa jina Maarufu anajulikana kama Eddy Kenzo amezaliwa huko Masaka nchini Uganda.  Mama yake alifariki kipindi ambacho Eddy alikua na miaka minne(4) tuu jambo ambalo lilimfanya msanii huyo kuanza kuishi mtaani na kuwa mtoto wa mtaana na hii ilitokana na Eddy kutokua anamfahamu baba yake wala ndugu yeyote kwa wakati huo na huko mtaani alikaa mpaka alipokuwa ana umri wa miaka 13.

Baada yakumaliza high school Eddy alijitwalia jina la kiusanii ambalo ni Eddy Kenzo na ndipo hapo akaanza kuandika muziki. Mnamo Mwaka 2008 alishirikishwa kwenye nyimbo ilijitwalia umaarufu nchin Uganda na Africa kwa ujumla wimbo uliokwenda kwa jina la "Yanimba" uliomilikiwa na msanii Mikie Wine.

Eddy Kenzo alizidi kujipatia umaarufu baada ya mwaka 2010 kuachia ngoma yake iliyokwenda kwa jina la "Stamina" ambapo wimbo huu aliutumia Rais wa Uganda Yoweri Museveni kipindi cha kampeni. Aliachilia Album yake ya kwanza mnamo mwaka 2012 iliyokwenda kwa jina la Ogenda Kunzisa na mwaka 2013 aliachilia album nyingine ilokwenda kwa jina la Kamunguluze na alifanikiwa kufanya toure nchini Marekani.

Wimbo wake wa "Sitya Loss" ndio wimbo uliozidi kumfanya Eddy awe maarufu Africa na Ulimwenguni kote na hasa pale alipowashirikisha gheto Kids wa Uganda kwenye video yake. Video hiyo ilipata kutazamwa kwa wingi na ilikua ikitazwa mara 10,000 kwa siku. Hivyo album yake ya tatu iliyokwenda kwa jina la "Sitya Loss" aliachilia mnamo mwaka 2014.

Eddy aliwahi kushirikishwa na kutambuliwa katika tuzo zifuatazo:
          RAWMA International Reggae and World Music Awards 2014 Nominee
         Channel O – Best East African Artist Nominee 2014
         AFRIMMA Awards –  Best Upcoming Artist Nominee 2014
         Kunde Awards –  Best East African Artist Winner 2014/2015
        Zina Awards –  Artist of the Year 2014/2015
        Rising Star Awards –  Song and Video of the Year 2014/2015
       BET Awards – Best New International Act Viewers Choice
Kwa  sasa anatamba na vibao vyake kama vile "SORAYE" na "ROYAL" ambapo katika wimbo huo wa "ROYAL" kamshirikisha msanii Patoranking.
Tazama nimbo yake ya "SORAYE" hapo chini Pia tizama video yake inayotamba kwa  sasa inayokwenda kwa jina la "ROYAL" ambapo kamshirikisha msanii Patoranking.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...