Michuano ya klabu bingwa Ulaya itaendelea tena leo kwa michezo miwili kuchezwa ikiwa ni nafasi ya kusaka tiketi ya robo fainali.
Miamba
wa soka wa Hispania Real Madrid, watakuwa nyumbani katika uwanja wao wa
Santiago Bernabeu kuwaalika As Roma, ambapo Real Madrid wanashuka
dimbani wakiwa na faida ya ushindi wa mabao 2-0 walioupata katika mchezo
wa kwanza. Katika dimba la Volkswagen Arena huko Ujerumani VfL
Wolfsburg watakipiga na Kaa Gent kutoka ubelgiji,VfL Wolfsburg wapo
katika nafasi nzuri kutinga Robo Fainali baada ya kushinda Mechi za
Ugenini kwa 3-2. Michezo hii itachezwa saa 4:45 kwa saa za Afrika
mashariki, Fainali ya michuano hii zitafanyika Mei 28 katika dimba la
San Siro huko Milan Itali.
08 March, 2016
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7
KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...

-
Brit Awads 2016 zimefanyika huko London ambapo mwanamuziki Adele ameondoka na tuzo nyingi zaidi katika nomination alizo kuwepo. Hizi hapa...
-
Mboga za majani na matunda zimekuwa zikisisitizwa kwa sana na wataalamu wa afya hasa kwa wanawake wajawaziti kwani zimekuwa zikiongeza Damu...
-
Yule mkali wa Rnb Rama Dee katuletea ngoma mpya "Kipenda Roho" Bofya ku Download Music: Rama Dee - Kipenda Roho.
No comments:
Post a Comment