Maafisa wa Umoja wa mataifa waliofanya uchunguzi huo wanasema raia wa Syria ambao wamekuwa wakiunga mkono waasi au kuipinga serikali wamekuwa wakikamatwa hapo hapo.
Wakati huo huo Wakati Majeshi Syria yakiendelea na mapambano katika mji wa Allepo, Uturuki imesema kipaumbele chake cha kwanza ni kuwapa misaada wale waliokimbia makazi yao kutokana na vita.
Naibu Waziri Mkuu Numan Kurtulmus amesema raia wa Syria wapatao elfu sabini na saba wanapatiwa msaada na Uturuki katika kambi katika eneo la mpakani.
Naye Waziri wa mpito wa Syria Hussein Bakri ameelezea kusikitishwa na kutokana na hali ilivyo"Haya ni mashambulizi ya mabomu yasiyo ya kawaida. Yamesababisha watu zaidi ya sabini elfu kukimbia makazi yao katika mji wa Alleppo kwa ujumla, na hasa eneo la kaskazini.Kama hali itaendelea kama hivi sasa, itasababisha watu zaidi laki nne kutoka Jimbo la Allepo na mji wa Allepo pekee kukimbia makazi yao. Ni wazi kabisa Urusi imedhamiria kuuzunguka na mji wa Allepo, kama ilivyotokea katika maeneo mengine ya Syria..
CHANZO=(BBC )
No comments:
Post a Comment