18 February, 2016

Albamu ya Kanye west yapakuliwa mara 500,000


Albamu mpya ya mwanamuziki Kanye West imepakuliwa kutoka mtandaoni zaidi ya mara 500,000 kulingana na kampuni ya kupakua kanda za video na sauti Torrent Freak.
Msanii huyo alitoa albamu hiyo ya Life of pablo kutoka kwa huduma ya mtiririko wa muziki wa Jay-Z Tidal siku mbili zilizopita.
Maelfu ya raia waliolipa ili kusikiza albamu hiyo walilalama kwamba wameshindwa kupakua albamu hiyo licha ya kuilipia.
Kwa sasa inaongoza miongoni mwa albamu zinazopakuliwa mitandaoni kwa njia ya wizi.
Albamu hiyo imeonekana mara mbili katika mtandao wa usambazaji wa miziki kumi bora iliopakuliwa,licha ya Kanye West kutuma ujumbe katika tweeter akisema kuwa albamu hiyo itapatikana katika Tidal pekee.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...