09 January, 2016

VITU VYA KUJIFUNZA PALE UNAPOSHINDWA KUFANIKIWA

Tambua kwamba mafanikio hayatoki mbali na wewe, hivyo basi jitahidi sana kufanya vitu ambavyo vinakuweka karibu na mafanikio

Kutengeneza mafanikio katika maisha huchukua muda mrefu hivyo basi jitahidi sana kuangalia jinsi ambavyo unafanya mambo yako kuwa na imani kwamba ipo siku utaona nguvu zako zimekulipa.

Tambua kwamba watu waliofanikiwa hufanya maamuzi magumu, hivyo basi jitahidi kuwa na msimamo katika maisha fanya maamuzi katika kila sekta.

Jifunze kutokana na makosa pia tambua kwamba mafanikio huja baada ya kuona na kukabiliana na hayo makosa au changamoto.

Watu wanaokuwa na wewe katika mafanikio ni wengi sana ila tambua sana watu wanaokuwa na wewe katika matatizo au changamoto za maisha ni wachache na hao ndio wale marafiki zako wa kweli.

Ni vigumu kufanikiwa kwa kufanya vitu ambavyo hupendi hivyo basi siku zote fanya vitu ambavyo unavipenda kama kazi na mafanikio utayaona.

Jiunge na watu 3000 walio chagua MTOKAMBALI ili kupata Makala zetu Kila week end moja kwa moja kwenye simu yako BURE!

* indicates required

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...