16 January, 2016

Mshambuliaji wa West Ham Andy Carroll huenda akakaa nje kwa muda wa wiki sita baada ya kuumia misuli ya paja.

Carroll
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 aliondolewa uwanjani baada ya kucheza dakika 15 pekee mechi dhidi ya Bournemouth, ambayo walishinda 3-1.
Carroll, 27, alikuwa amewafungia West Ham mabao mawili katika mechi zake nne za majuzi zaidi baada ya kurudi kucheza Septemba 2015.
Kabla ya hapo, alikuwa amekaa miezi saba nje baada ya kufanyiwa upasuaji kwenye goti lake.
“Mambo yakienda tunavyotarajia, basi atatusaidia mechi 10-15 za mwisho msimu huu,” amesema meneja wa West Ham Slaven Bilic.
Carroll, ambaye aliwahi kuchezea Newcastle, Carroll alijiunga na West Ham kutoka Liverpool kwa £15m mwezi Juni 2013.
West Ham wamo nambari tano ligini, alama moja pekee nyuma ya Tottenham walio nambari nne, zikiwa zimesalia mechi 17 za kuchezwa msimu huu.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...