15 December, 2015

Hoteli iliyoshambuliwa Mali kufunguliwa

Mali
Hoteli iliyoshambuliwa katika mji mkuu wa Mali, Bamako, mwezi jana itafunguliwa tena leo.
Watu wenye silaha walishika mateka wageni 170 kwa saa tisa katika hoteli ya Radisson Blu, na kuua watu 22 na kujeruhi wengine 14.
Polisi na wanajeshi wa Mali, wakisaidiwa na vikosi vya usalama kutoka nje, waliingia kwenye hoteli hiyo na kuwaua washambuliaji.
Rais wa Mali Ibrahim Boubacar Keita ametangaza kupitia Twitter kwamba hoteli hiyo itafunguliwa.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...