17 December, 2015

Guardiola Akiondoka Bayern: Je atakwenda Etihad, Old Trafford au Darajani?

Kocha huyo mwenye sifa kubwa miongoni mwa makocha bora duniani ameiambia Bayern Munich kwamba hana mpango wa kuongeza mkataba wake mwishoni mwa msimu.
Vilabu tofauti ulimwenguni ikiwemo Barcelona, ambapo kocha hugo alishinda mara mbili  Champions League pamoja na makombe matatu ya La Liga, wapinzani wao Real Madrid nao pia wanaonekana kuvutiwa baada ya kuonekana wana nia ya kuachana na Rafa Benitiez.
  Lakini inaonekana hatma ya Kocha huyo itaamuliwa na vilabu vya England, Chelsea, Manchester United na Manchester City wote wanaonekana kumtaka kocha huyo mwenye rekodi nzuri ya makombe.
Arsenal pia inaweza kuhusika ikiwa Guardiola ataamua kupumzika mpaka mkataba wa Wenger utakapomalizika mwishoni mwa msimu ujao.
Guardiola alitoboa siri kwenye kitabu chake   “Pep Confidential” kwamba, baada ya kuondoka Barcelona na kabla hajaamua kujiunga na Bayern, alikuwa na nafasi ya kujiunga na City na Chelsea.
Manchester United pia walidhaniwa kwamba walikuwa wanamtaka Guardiola kabla ya kumuajiri  Louis Van Gaal.
Sasa inaonekana  United wanaweza kuachana LvG, na wanapewa nafasi ya kumtwaa Guardiola ambaye anatajwa kuvutiwa na utamaduni wa United hasa katika matumizi ya kutumia academy yao.
Kadri siku zinavyoenda ndivyo inavyoonekana ngumu kwa Van Gaal kuweza kumaliza misimu yake mitatu ya mkataba wake – mashabiki na inaripotiwa baadhi ya wachezaji wameanza kumpinga.
  Guardiola pia amekuwa akihusishwa kwa muda na kuhamia Etihad, wengi wakitoa sababu ya uhusiano wake na CEO wa City Ferran Soriano na mkurugenzi wa soka Txiki Begiristain ambao walifanya nae kazi Barcelona.
Lakini baadhi ya vyombo vya habari Uingereza vinaeleza kwamba Guardiola ataichagua United mbele City ikitokea United wakionyesha nia ya dhati ya kumhitaji.
Carlo Ancelotti anatajwa kwamba ndio mrithi wa Guardiola ndani ya Allianz Arena

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...