22 June, 2015

Ben Pol kuachilia album yake akiwa chini ya uongozi mpya wa Panamusiq

Pamoja na wasanii wa Tanzania kuonesha kusita kutoa album zao sokoni, Ben Pol amesema mwaka ujao atatoa yake akiwa chini ya uongozi mpya wa Panamusiq.Muimbaji huyo wa Sophia amesema kuanzia mwezi wa kwanza mipango hiyo inaweza kuanza rasmi.
“Mwezi kwanza tunaanza promotion ya album ambayo itatoka mwezi wa sita au mwezi wa 12 mwakani kwahiyo hii ni project ya mwakani.”Hivi karibuni Ben Pol alisafiri kwenda nchini Ujerumani kwenda kufanya video ya wimbo wa msanii wa Tanzania aishiye nchini humo aliyemshirikisha, Emanuel Austin.
Kwa sasa msanii huyo yupo jijini Nairobi, Kenya alikoenda kurekodi kipindi cha Coke Studio Afrika.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...