17 May, 2015

EPL: Man u na Arsenal zatoka sare nA HUU ni msimamo wa ligi hiyo;

28C9867D00000578-3085329-image-a-74_1431881272464
Herrera akifunga goli lake
MANCHESTER United ikiwa uwanja wa nyumbani wa Old Trafford imetoka sare ya 1-1 dhidi ya Arsenal katika mechi ya ligi kuu England iliyomalizika usiku huu.
Ander Herrera katika dakika ya 30′ alipata pasi nzuri kutoka kwa Ashley Young na kuifungia Manchester United bao la kuongoza.
United wakiwa na matumaini ya ushindi, dakika ya 82′ Tayler Blackett aliyetokea benchi alijifunga goli katika harakati za kuokoa na kufanya mechi hiyo imalizike kwa sare hiyoMarouane Fellaini (left) and Ashley Young (right), who both played a part in the build-up to the goal, celebrate with Herrera
Kama ilivyo kawaida kwa mechi za karibuni, United waliongoza umiliki wa mpira kwa 58% dhidi ya 42% za Arsenal.
Mbali na hilo, United wamepiga mashuti 6 dhidi ya 4 yaliyolenga lango, wakati ambayo hayakulenga lango, mashetani wekundu wamepiga 6 dhidi ya 2 ya Gunners.
Hata hivyo kila timu imepiga kona 5 katika mechi hiyo iliyovuta hisia za mashabiki wengi.Theo Walcott crosses, and the ball is deflected off the unfortunate Tyler Blackett to bring Arsenal level at Old TraffordMatokeo haya yanaonesha wazi kuwa Man United watamaliza nne bora, wakati Arsenal watamaliza nafasi ya pili na Man City nafasi ya tatu.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...