04 April, 2015

YANGA YATINGA 16 BORA>>>>>>>

YANGANAPLATINUM1
Maabingwa wa zamani wa ligi kuu ya Tanzania bara, ambao ni wawakirishi pekee wa Tanzania katika michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika, Dar es Salaam Young Africans, leo wamefanikiwa kusonga mbele katika hatua ya 16 bora ya michuano hiyo licha ya kufungwa bao 1-0 dhidi ya FC Platinum.
Yanga ambao walikuwa na faida ya bao 5 ambazo walizipata katika mchezo wa kwanza uliopigwa Jijini Dar Es Salaam wiki mbili zilizopita, leo walijikuta wakifungwa na wenyeji hao kupitia kwa W. Musona kunako dakika ya 30 kipindi cha kwanza kwa shuti kali akiunganisha krosi safi kutoka upande wa kushoto.
Katika mchezo huo Platinum walikuwa wakishambuia kwa wingi lango la Yanga huku Watanzania hao wakifanya mashambulizi ya Kushitukiza, ambapo dakika ya 4 Platinum Walipata bao lakini muamuzi akalikataa kwasababu tayari mchezaji alikuwa amekwisha otea.
Dakika ya 12 Kipa wa Yanga Ally Mustafa Bartez aliisaidia Yanga baada ya kuokoa mchomo uliopigwa langoni huku mshambuliaji wa Platinum akiwa na kipa lakini kipa huyo akapangua na kufanya Yanga waanze upya kujipanga.
Mshambuliaji wa Yanga Mrisho Halfani Ngassa alikosa bao kunako dakika ya 22 baada ya ‘kukunjuka, kupiga Tik-Tak ambayo haikuzaa matunda kufatia kichwa cha Amis Tambwe aliyeunganisha mpira wa kona uliopigwa na Simon Msuva.
Hadi muamuzi anapuliza kipenga cha mwisho kuashiria kipindi cha kwanza kimemalizika Yanga walikuwa Nyuma kwa bao 1-0 lililofungwa na Musona.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo kocha wa Yanga Hans Van Pluijm aliamua kumtoa beki Said Juma Allly na nafasi yake akaingia mkongwe Calvin Yondani ili kuhakikisha Platinum hawapati bao linguine na kuwaweka Yanga katika wakati mgumu.
Dakika ya 53 Mrisho Ngassa anakosa bao la wazi baada ya kupenyezewa pasi na Kiungo Haruna Niyonzima lakini Uncle akawa kwenye kizingiti cha mabeki wa Platinum ambao waliokoa mpira huo.
Simon Msuva kunako dakika ya 55 aliwakosesha Yanga bao baada ya kuwaadaa mabeki wa Platinum na kuachia shuti kali ambalo pia halilkuleta madhara na kugeuka mboga kwa kipa wa Platinum.
Ili kuhakikisha labda wanapata angalau bao la ugenini hata moja Kocha Hans Van Pluijm aliamua kumpumzisha Msuva na nafasi yake kuchukuliwa na Dan Mrwanda kunako dakika ya 89.
Baada ya dakika 4 za nyongeza Mrisho ngasa alipewa kadi ya Njano kwa kumchezea vibaya mchezaji wa Platinum ikiwa ni pamoja na kupinga maamuzi ya Refa.
Hadi dakika ya mwisho Yanga wanauwa wamefanikiwa kusonga mbele kwa jumla ya mabao 5 kwa 2 kwani mchezo wa awali matokeo ilikuwa 5 kwa Yanga na 1 kwa Platinum.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...