11 April, 2015

kurasa za MAGAZETINI TZ leo April 11 2015,

 
NIPASHE
Mbunge wa zamani wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Mussa Lupatu ni miongoni mwa waliofariki katika ajali ya mabasi mawili na gari ndogo iliyotokea kijiji cha Mkata Tanga.
Kaimu Kamanda wa Polisi Tanga, Juma Ndaki amesema Marehemu Lupatu alipata ajali hiyo akitokea Kibaha kuelekea Korogwe kumpeleka mwanae kupatiwa matibabu ya ugonjwa akili ambaye naye pia alifariki.

Wengine waliyotajwa kufariki katika ajali hiyo ni karani wa Mahakama ya Ardhi Dar es Salaam, Devota Msimbe ambaye alifariki wakati akikimbizwa Hospitali ya Muhimbili.
Kamanda Ndaki alisema maiti tatu bado hazijatambuliwa na miili yao imehifadhiwa katika hospitali ya Magunga Korogwe, majeruhi 12 bado wamelazwa katika Hospitali tofauti.
Majeruhi 12 kati ya 34 wamelazwa katika hospitali tofauti, wakiwamo saba waliopelekwa Muhimbili, mmoja hospitali ya wilaya ya Handeni na wanne kituo cha afya Mkata, wilayani Handeni.
NIPASHE
Watu wanaoishi Vigwaza, wilaya ya Bagamoyo wameamua kuwaajiri watoto wao waliomaliza kidato cha nne kufundisha Shule ya Msingi Visezi, ili kutatua tatizo la upungufu wa walimu shuleni hapo huku wakiwalipa posho ya sh. 15,000 kwa wiki.
Wananchi  hao wamesema wanawalipa watoto hao Sh. 15, 000 kwa wiki kama posho ya kujikimu.
Walisema wameamua kuajiri watoto wao baada ya kuona wamekuwa na changamoto hiyo kwa aidi ya miaka 10 na hakuna juhudi zozote zinazofanywa na serikali kutatua tatizo hilo.
Ngoja tukwambie, sisi wanavisezi wote ni wanaCCM kwa hiyo usiwe na wasiwasi lakini kama hutatatua hizi kero zetu CCM itashinda kwa shida sana, sio siri,”—alisema Mwenyekiti wa kijiji hicho, Hamisi Kiatala.
“Kero ya walimu itakwisha hivi karibuni.. TAMISEMI wana mpango wa kuwaajiri walimu, lakini viongozi wa kijiji hamjawahi kuniambia hizi kero zenu wakati mimi ni mbunge wenu pia ndio waziri mwenye dhamana… hizi kero zinazowezekana kutatua nitazitatua kwa kushirikiana na viongozi wa kijiji, zitakazoshindikana tutazishughulikia mwakani kama nitarudi tena”, alisema Kiatala.
HABARI LEO
Kusambaa kwa taarifa kuwa kuna uwezekano wa kutokea kwa shambulio la kigaidi katika miji ikiwemo Dar na Mwanza kumefanya baadhi ya Taasisi kama vyuo vikuu na TANESCo kuchukua tahadhari kwa kuweka taarifa ya tahadhari na kuelekeza namna hatua za kufanya ili kujiepusha na kujilinda.
Kutokana na tishio hilo, tumeona ni vyema tuchukue hatua mapema.. si lazima yatokee ndivyo tuchukue hatua, tumeona ni vyema kujihami kwa kuimarisha ulinzi katika vituo vyetu..”—Mkurugenzi wa TANESCo, Felchesmi Mramba.
Baadhi ya tahadhari walizozichukua Taasisi hizo ni wafanyakazi na wanafunzi kuvaa vitambulisho vyao wakati wote, ukaguzi wa wageni na watu wote wanoingia maeneo ya Taasisi hizo, pamoja na kuwekwa kwa matangazo ya tahadhari katika maeneo hayo.
Jeshi la Polisi limeonywa watu kuacha tabia ya kutunga na kusamba ujumbe kwenye simu na mitandao ya kijamii unaowatia hofu wananchi.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...