13 October, 2016

Mbio Za Kilimanjaro Marathon 2017 Zazinduliwa Dar Es Salaam.....Kufanyika Februari 26, 2017

Mbio za Kilimanjaro Premium Lager Marathon 2017 ambazo ni za 15 tangu Kuanzishwa kwake, zimezinduliwa rasmi  leo jijini Dar es Salaam katika mkutano na wanahabari, wadhamini na Chama Cha Riadha Tanzania.

“Tumeona matunda ya udhamini huu kwa mfano mwaka huu tumeshuhudia mshiriki wa Kili Marathon akishiriki katika michezo ya Olimpiki kule Brazil na kumaliza katika nafasi ya tano katika mbio za kilomita 42. Tunaweza kuwapata akina Simbu wengi kutoka kili Marathon na ndicho hasa wadhamini wengi wanakitafuta,” alisema Mkurugenzi wa Masoko wa TBL Group, Kushilla Thomas

Aidha Mkurugenzi huyo alisema  wadhamini wengine wa mashindano hayo ni Tigo ambao wanadhamini 21km, Gapco kwa 10 km-viti vya magurudumu na baiskeli ya kunyonga kwa mkono na Grand Malt-5km. Wadhamini wengine ni pamoja na KK Security, TPC Limited, FNB, Kibo Palace, Kilimanjaro Water, CMC Automobile,Keys Hotel, Air Rwanda na Anglo Gold Ashanti.
 
Aliishukuru pia  wizara yenye dhamana ya michezo kwa kuhakikisha miaka yote kwamba tukio hili linafanikiwa,pia amewapongeza waandaaji, Wild Frontiers, waratibu wa kitaifa-Executive Solutions, Chama cha Riadha Tanzania (RT), Kilimanjaro Marathon Club, Mkoa wa Kilimanjaro na Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) kwa kuwa wenyeji wa mashindano hayo.
 
Kwa upande wake, Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, Pamela Kikuli zawadi kwa 42km Kilimanjaro Premium Lager Marathon ni pamoja na – jumla ya Tsh milioni 20 kwa washindani wanaume na wanawake watakaoshika nafasi 10 za juu. Mshindi wa kwanza kutoka kila kundi atapata Tsh milioni 4 kila mmoja.

 “Hatuwezi kuwasahau wanariadha wote wa hapa nchini walioshiriki kwenye mashindano haya na kuipa fahari nchi yetu na kuwa watashinda zawadi zote hizi tunazozitoa. Tunaamini kwamba mashindano haya ya marathon pia yatafungua milango kwa wanariadha wetu kwa ajili ya kushiriki mashindano ya kimataifa ya marathon nje ya nchi yenye zawadi kubwa,” alisema Pamela Kikuli.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...