22 July, 2015

Louis Van Gaal amelalamikia kiwango kibovu alichokionesha kiungo wa kijerumani Bastian Schweinsteiger

bastian22july15-592891
Matarajio ya mashabiki wa timu mbalimbali za soka duniani ikitokea wachezaji wamesajiliwa na timu zao kwa ada kubwa ya uhamisho, wanasubiri kuona wachezaji hao wanafanya vizuri katika timu mapema.. na hali hiyo sio kwa mashabikio pekeyao ila hata Kocha wa Manchester United Louis van Gaal.
CKgL41qUEAEImuv
Licha ya ushindi wa goli 3-1 walioupata Man United dhidi ya San Jose Earthquakes, kocha wa Man United Louis Van Gaal amelalamikia kiwango kibovu alichokionesha kiungo wa kijerumani Bastian Schweinsteiger ambaye amesajiliwa msimu huu akitokea FC Bayern Munich ya Ujerumani kwa ada ya uhamisho inayokadiriwa kufikia pound milioni 15.
bastian-schweinsteiger-manchester-united-football_3326624
“Mchezaji anaweza kucheza vibaya kama amefanya mazoezi kwa siku tatu hadi sita, lakini anaweza kumudu kucheza kwa dakika 45. Schweinsteiger alicheza vibaya, nafikiri mechi ya kwanza alicheza vizuri ila kwa hii amecheza vibaya”>>>Louis van Gaal
International-Champions-Cup-2015-Club-America-v-Manchester-UnitedTazama magoli yote ya Manchester United na Highlights za mechi:

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...